Swali. Kwa kutumi mifano ainisha ngeli za nomino za
Kiswahili kwa kigezo cha kimofolojia kisha
jadili upungufu wa uainishaji huo.
Istilahi Ngeli imechukuliwa kutoka ligha ya kihaya
(Tanzania). Katika lugha ya kihaya neno ngeli lina maana ya aina ya kitu.
Tuki (1990), wanaeleza kuwa Ngeli za nomino ni kundi moja la
majina yaliyo na upatanisho wa kisarufi unaofanana na viambishi vya umoja na
wingi vinavyofanana. Kwa mujibu wa fasili hii ngeli za nomino ni kundi la
nomino zilizo na:
·
Upanisho
wa kisarufi unaofanana (kisintaksia), na
·
Viambishi
vya umoja na wingi vinavyofanana (kimofolojia).
Kamusi ya Kiswahili sanifu (1981), inaeleza kuwa ngeli za
nomino ni utaratibu wa taaluma ya sarufi ya lugha katika kupanga aina za
majina. Fasili hii ina upungufu kwa sababu tunaamini kuwa ngeli ni kundi la
nomino za aina moja na ndio ule utaratibu wa kupanga nomino katika makundi kama
fasili ya hapo juu inavyodai.
Kwa ujumla ngeli za nomino ni utaratibu unaotumika kupanga
nomino za lugha katika makundi mbalimbali kwa kufuata vigezo vya kisarufi
katika lugha ya kiisimu.
Kigezo cha kimofolojia ni kigezo ambacho huzingatia zaidi
viambishi awali vya umoja na wingi lakini mzizi na viambishi tamati
havihusishwi. Nomino zilizo na viambishi vya mwanzo vilivyosawa huwekwa katika
ngeli moja. Ngeli za nomino huwa na sehemu mbili kimuundo ambazo huwa ni mwanzo
na shina. Mwanzo huwa ni kiambishi awali na shina hujumuisha mzizi wa neno na kiishio
ambacho huwa ni mofimu inayotumiwa kuunda nomino. Kiambishi awali ambacho
hutumika kuainishia ngeli huitwa kiambishi ngeli.
Kwa kutumia kigezo cha kimofolojia ngeli za nomino za
Kiswahili zimeainishwa katika makundi mbalimbali kwa kurejelea hali ya umoja na
wingi wa nomino husika. Katika kigezo hiki kila kiambishi ngeli hupewa namba ya
kukitambulisha. Kigezo hiki kimejadiliwa na wataalamu mbalimbali na miongoni
mwao ni Mgullu na Habwe na Karanja.
Kwa kuanza na Mgullu (2001), katika kuainisha ngeli za nomino
anazingatia zaidi viambishi awali vya idadi ya umoja na wingi katika nomino
hizo. Mzizi na viambishi tamati katika nomino hizo huwa havihusishwi hata
kidogo. Aidha viambishi awali vinavyotumika ni vile vya umbo la kawaida la
nomino siyo viambishi awali vya ukubwa au udogo wa nomino hizo. Ngeli
tutakazopata hapa zitakuwa ngeli za nomino za kimofolojia tofauti na ngeli za
nomino za kisintaksia. Kwake yeye kundi moja la nomino zilizo na viambishi
awali vya umoja na/au wingi vinavyofanana au nomino zilizo na viambishi awali
hata kimoja huwa na ngeli yao. Yeye aliainisha makundi makuu manne ya ngeli za
nomino kimofolojia ambayo ni; ngeli sita za nomino zilizo na viambishi awali
vyote viwili yaani umoja na wingi, ngeli moja ya nomino zilizo na kiambishi
awali cha umoja tu pamoja na mofu kappa ya wingi, ngeli moja ya nomino zilizo
na kiambishi awali cha wingi tu pamoja na mofu kapa ya umoja, na ngeli moja ya
nomino zisizo na kiambishi chochote. Kwa ujumla anaainisha ngeli za nomino tisa
ambazo ni kama ifuatavyo:
1)
Ngeli
ya MU-WA
Katika ngeli hii zipo nomino zilizo na kiambishi awali {MU} katika
umoja na kiambishi awali {WA} katika wingi. Kwa mfano
Umoja
wingi
Mu + tu (mtu)
watu
Mutoto (mtoto) watoto
Muungwana waungwana
Muana
(mwana) wana
Mofu (MU) ya umbo halisi la umoja katika ngeli huweza
kudhihirishwa katika maumbo mbalimbali kama vile {M, MU na MW}.
2)
Ngeli
ya M-MI
Ngeli hii ina nomino ambazo hutumia kiambishi awali {M}
katika umoja na {MI} katika wingi.
Kwa mfano; umoja wingi
M
+ ti mi
+ ti
M
+ tume mi
+ tume
M
+ chungwa mi
+ chungwa
M
+chezo mi
+ chezo
3)
Ngeli
ya JI-MA
Katika ngeli hii zipo nomino zilizo na kiambishi awali cha
umoja {JI} na kiambishi awali cha wingi {MA}. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Jicho macho
Jiwe mawe
Jino meno
Jiko maiko
(meko).
4)
Ngeli
ya KI-VI
Katika ngeli hii zipo aina za nomino zilizo na kiambishi
awali cha umoja {KI} na kiambishi awali cha wingi {VI}. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Kiti viti
Kiatu viatu
Kiumba
(chumba) viumba
(vyumba)
Kiakila
(chakula) viakula
(vyakula).
Hapa umbo {KI} kiambishi awali cha umoja, lina alomofu mbili
yaani {Ki} na {Cha} na umbo {VI} la wingi lina alomofu {Vi} na {Vy}.
5)
Ngeli
ya U-N
Katika ngeli hii kuna nomino zenye kiambishi awali {U} umoja
na {N} wingi. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Udevu ndevu
Udago ndago
Udara ndara
Ulimi ndimi
Ubawa mbawa
Tunaona hapa kuwa {N} umbo la wingi lina alomofu mbili yaani
{N} na {M} katika muktadha maalumu.
6)
Ngeli
ya U-MA
Katika ngeli hii {U} ni kiambishi cha umoja na {MA} ni
kiambishi cha wingi. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Ugonjwa magonjwa
Uasi maasi
Upishi mapishi
Uamuzi maamuzi.
7)
Ngeli
ya U- Ø
Ngeli hii hujumuisha maneno ambayo kiambishi awali umoja huwa
ni {U} na kiambishi awali wingi mofu kappa{ Ø}. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Ukuta Ø
+ kuta (kuta)
Ukucha Ø
+ kucha (kucha)
Upande Ø
+ pande (pande).
8)
Ngeli
ya Ø-MA
Katika ngeli hii mofu kappa { Ø} huwakilisha umoja na mofu
{ma} huwakilisha wingi. Kwa mfano:
Umoja
wingi
Ø
debe madebe
Ø
kasha makasha
Ø
jembe majembe
Ø
bepari mabepari.
9)
Ngeli
ya Ø-Ø
Nomino zilizo katika ngeli hii ni zile ambazo hazina
kiambishi idadi hata kimoja. Maumbo ya nomino hizi hayaoneshi idadi (umoja na
wingi) katika maumbo yake. Kwa mfano:
Umoja wingi
Taa taa
Saa saa
Kuku kuku
Ng’ombe ng’ombe
Nyumba nyumba
Samaki samaki.
Baada ya kuona uainishaji wa ngeli za nomino kwa kutumia
kigezo cha kimofolojia kwa mujibu wa Mgullu, tutazame uainishaji wa ngeli hizi
kwa kutumi kigezo hikihiki cha kimofolojia kwa mujibu wa Habwe na Karanja
(2012). Wao wanaainisha ngeli za nomino kwa kuzingatia kufanana kwa viambishi
vya mianzo ya nomino. Nomino zenye viambishi awali vilivyosawa huwekwa katika
ngeli moja. Wao wanaainisha ngeli zifuatazo:
1.
Ngeli
ya {MU}
Ngeli hii huchukua nomino zenye kiambishi ngeli {mu} pamoja
na alomofu zake.
Kwa mfano; {MU} m- motto, mtu,
mu- muungwana, muuaji na
mw- mwalimu.
2.
Ngeli
ya {WA}
Hii ni ngeli yenye kundi la wingi wa ngeli ya kwanza. Kwa
mfano:
{WA}
- watoto, watu, waungwana, wauaji na waalimu.
3.
Ngeli
ya {M}
Ngeli hii ni ya umoja ambayo pia ina alomofu zake tatu yaani
m, mu na mw. Kwa mfano:
Mut
i- mti
Muembe
- mwembe
Mundi
– mundi.
{mw} hutokea ikiwa shina la nomino linaanzia na vokali [u],
huwa {m} ikiwa shina la nomino linaanza na konsonanti na huwa {mu} ikiwa shina
la nomino linaanza na vokali [u].
4.
Ngeli
ya {MI}
Ngeli hii huchukua wingi wa ngeli ya tatu. Kwa mfano:
Miti,
migomba, miembe na miundi.
5.
Ngeli
ya {JI/Ø}
Mofu ya ngeli hii huwa ni {ji}. Kwa mfano jitu, jicho, Øgoti,
na Øtawi. Kuna nomino zingine huunganishwa katika kundi hili japo hazina umbo
dhahiri lililotajwa kwa maana zina mofu kapa. Nomino hizi huunganishwa katika
kundi hili kwa sababu zenyewe wingi wake unaingiliana na ule wa kundi hili
unaodhihirishwa katika ngeli ya sita.
6.
Ngeli
ya {MA}
Ngeli hii huwakilisha wingi wa ngeli ya tano. Kwa mfano:
macho, magoti, matawi na majitu.
7.
Ngeli
ya {KI}
Mofu ngeli {ki} huwa na alomofu {ch} kutokana na kanuni za kifonolojia
(ukaakaishaji). Kwa mfano nomino katika kundi hili ni: kiatu, kitu, kisu na
kiakula (chakula).
8.
Ngeli
ya {VI}
Ngeli hii huonesha wingi wa ngeli ya saba kwa mfano viatu,
vitu, visu na viakula (vyakula). Ngeli hii ina alomofu {vy}.
9.
Ngeli
ya {N/Ø}
Ngeli hii huhusisha majina yanayoanza na N na kufuatiwa na
konsonanti. Kwa mfano nyumba, nguzo na nguo.
10. Ngeli ya {N/Ø}
Ngeli hii huwakilisha wingi wa ngeli ya tisa {n} japokuwa
hakidhihiriki kaika maneno mengi ya ngeli hii. Ngeli ya tisa na kumi
hudhihirika zaidi kisintaksia na siyo kimofolojia tu.
11. Ngeli ya {U}
Nomino zenye kiambishi cha umoja {u} kwa mfano ulimi na
ugonjwa huingia katika kundi hili. Pia ngeli hii ina alomofu {w} kwa mfano
maneno kama: uembe (wembe) na uaraka (waraka).
12. Ngeli ya {KA} kwa mfano katoto na
kagari.
13. Ngeli ya {TU}
Ngeli hii inawakilisha wingi wa ngeli ya 12. Kwa mfano: tu +
toto na tu + gari. Pia ngeli hii huwa na
alomofu {tw}. Kwa mfano: twana na twalima (tuana na tualima).
14. Ngeli ya {U} kwa mfano u + zuri na u
+ tukufu.
15. Ngeli ya {KU}
Ngeli hii hurejelea vitenzi vinavzofanya kazi kama nomino.
Kwa mfano: kuimba, kucheza na kuruka.
16. Ngeli ya {PA}
Ngeli hii huonesha mahali kamili au mahususi kwa mfano: pale,
ndani na hapa.
17. Ngeli ya {KU}. Ngeli hii huonesha
mahali kwa ujumla kwa mfano huku.
18. Ngeli ya {MU}. Ngeli hii huonesha
undani wa mahali kwa mfano humu, na mule.
Baada ya kuona uainishaji wa ngeli za nomino kwa kutumia
kigezo cha kimofolojia kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali, ufuatao ni upungufu
wa kigezo hiki:
Muingiliano wa ngeli kwa mfano ngeli ya 1. Umoja na ya 2.
Umoja ambapo kiambishi au mofu yake ni {m}. Kwa mfano katika maneno kama vile:
mtu, mwana, mtoto na muungwana katika ngeli ya kwanza umoja na mti, mtume,
mchungwa na mkono katika ngeli ya pili. Hali hii ya muingiliano inatokea pia
katika ngeli ya 3 na 6 wingi, na ngeli ya 5, 6 na 7 umoja. Hii ni kwa mujibu wa
mgullu (2001).
Kuna baadhi ya ngeli zinaonesha kiambishi kimoja tu aidha cha
wingi au umoja. Kwa mfano kwa mujibu wa uainishaji wa Mgullu (2001) katika
ngeli ya 7. {U- Ø} na ngeli ya 8. { Ø-MA}. Ngeli hizi hazina viambishi vya
upande mmoja kwa mfano katika ngeli ya saba wingi na ngeli ya nane umoja.
Ngeli ya 9. (Ø - Ø) kwa mujibu wa mgullu (2001) haina
kiambishi chochote aidha cha umoja au wingi. Huu ni udhaifu mwingine kwa kua
msingi wa uainishaji huu (uainishaji wa kimofolojia) huzingatia viambishi awali
vya umoja na wingi katika nomino ambavyo hufanana na kisha kuziweka nomino hizo pamoja katika ngeli moja.
Uainishaji huu unachanganya nomino zisizo na uhai na zile zenye
uhai. Kwa mfano kwa mujibu wa Mgullu (keshatajwa), katika ngeli ya nne kuna
majina ya viumbe wenye uhai na vitu visivyo na uhai kwa mfano: kiti/viti,
kiatu/viatu na kiumba (chumba)/viumba (vyumba) hizi ni nomino za vitu visivyo
na uhai. Kwa upande mwingine nomino za vitu vyenye uhai ambazo huwekwa katika
kundi hili ni kama vile: kiongozi/viongozi, kipofu/vipofu, kilema/vilema na
kijana/vijana.
Kigezo hiki kinajihusisha na maumbo ya umoja na wingi tu na
kutupilia mbali upatanisho wa kisarufi.
Pia udhaifu mwingine wa uainishaji wa ngeli za nomino kwa
kutumia kigezo hiki cha kimofolojia, wataalamu wanatofautiana katika idadi ya
ngeli. Kwa mfano Mgullu (keshatajwa) anaainisha ngeli tisa wakati Habwe na
Karanja (wameshatajwa) wanaainisha ngeli kumi na nane.
MAREJELEO
Habwe, J. & Karanja, P. (2012). Misingi ya Sarufi ya
Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers.
Mgullu, R.S. (2001). Mtalaa wa isimu. Nairobi: Longhorn
Publishers Ltd.
No comments:
Post a Comment